Waimbaji wa Nyimbo za Injili Tanzania, J Sisiters wakifanya Mahojiano na Dada Mary Damian wa Strictly Gospel
Ni ndugu wa familia moja Juliana Mshamma, Jacqueline Mshamma, Jessica Mshamma na Jennifer Mshamma kwa pamoja wameunda kundi lao wanajiita J SISTERS kwasababu herufi za majina yao ya kwanza zinaanza na J. Wanajulikana sana kwa umahiri wao wa kucheza na utunzi wa nyimbo za kipekee zinazowatambulisha kama J SISTERS, Album yao ya kwanza BADO KIDOGO ndiyo iliyowatambulisha vyema kwenye muziki wa Injili Tanzania na nje ya nchi! Album ya Pili SHUKA BWANA ilifanya vyema na wakafikiria kutoka kimataifa na album ya tatu TAKE THE VICTORY imewafanya wafikirie kufika mbali kimuziki na katika utumishi Mungu aliowaitia.
Pichani Juu: Julie, Jacqueline na Jennifer wakiwa maeneo ya Chuo wanachosoma Liberty, USA. Nyimbo zao zinapatikana sokoni na walio nje ya Tanzania hususan USA wanaweza kupata nyimbo zao kwa kuwasiliana nao kwa simu +434 426 2267
MAHOJIANO ZAIDI SIKILIZA HAPA!
Filed under: SINGERS
