Quantcast
Channel: Strictly Gospel » SINGERS
Viewing all articles
Browse latest Browse all 31

Waimbaji wa nyimbo za Injili ni wanafki – Stara Thomas

$
0
0

Mwimbaji wa zamani wa Bongo fleva ambae sasa ni mwimbaji wa nyimbo za Injili Stara Thomas hivi karibuni alitaja sababu za kushindwa kushirikiana na waimbaji wengine wa nyimbo za Injili kwenye album yake ya kwanza iliyo sokoni sasa.

Aliongea haya alipokuwa akihojiwa kupitia AMPLIFAYA na Millard Ayo  “kwenye upande wa Injili waimbaji wengi bado hawajawa na ufahamu wa kufanya kolabo japo lile ni neno la Mungu linalosimama peke yake haijalishi mnashirikiana au hamshirikiani lakini kushirikiana ni jambo jema, ugumu ambao nimeuona na nimejifunza ni kuhusu unafiki mkubwa sana, mtu anaweza kukuchekea machoni lakini moyoni ni muongo, kuna wengine wasanii wakubwa niliwaona nikafikiri lakini nilipowakaribia nikagundua sio, unafiki ni mwingi, kule kwenye bongofleva kulikua kuna upendo”

Na inasemekani hii sio mara ya kwanza Stara Thomas kutoa madai hayo, mwigizaji Dokii mwanzoni alipookoka, aliwahi kusema wazi waimbaji watano wakubwa wa Injili Tanzania,  ni wanafiki, wana ubinafsi, chuki, kujisikia na kujitenga na hawakukubali kumpa ushirikiano wowote.

Millard Ayo pia aliandika kwenye website yake kwamba waimbaji wa Gospel wenyewe wameshawahi kukiri kwamba hakuna upendo kati yao, watu wanachukiana, hawana umoja. Rose Muhando, Upendo Nkone na Miriam Mauki walishalisema hilo kwenye AMPLIFAYA ya CLOUDS FM.


Filed under: SINGERS

Viewing all articles
Browse latest Browse all 31

Trending Articles